Nehemia 6 Swahili & English
Listen/Download AudioNehemia 6 (Swahili) | Nehemiah 6 (English) |
---|---|
Basi ikawa, walipoarifiwa Sanbalati, na Tobia, na Geshemu, Mwarabu na adui zetu hao wengine, kwamba nimeujenga ukuta, wala hayakusalia mavunjiko ndani yake; (ijapokuwa hata wakati ule sijaisimamisha milango katika malango); Nehemia 6:1 |
Now it happened, when it was reported to Sanballat and Tobiah, and to Geshem the Arabian, and to the rest of our enemies, that I had built the wall, and that there was no breach left therein; (though even to that time I had not set up the doors in the gates;) |
Sanbalati na Geshemu wakatuma wajumbe kwangu, wakasema, Njoo, tukutane huko vijijini katika nchi tambarare ya Ono. Walakini wakakusudi kunifanyia mabaya. Nehemia 6:2 |
that Sanballat and Geshem sent to me, saying, Come, let us meet together in [one of] the villages in the plain of Ono. But they thought to do me mischief. |
Na mimi nikatuma wajumbe kwao, nikasema, Hii ni kazi kubwa ninayoifanya mimi, hata nisiweze kushuka; mbona kazi ikome, hapo ninapoiacha, niwashukie? Nehemia 6:3 |
I sent messengers to them, saying, I am doing a great work, so that I can't come down: why should the work cease, while I leave it, and come down to you? |
Nao wakaniletea maneno kama hayo mara nne; nikawajibu maneno kama yale. Nehemia 6:4 |
They sent to me four times after this sort; and I answered them after the same manner. |
Ndipo Sanbalati akamtuma kwangu mtumwa wake vile vile mara ya tano, na barua wazi mkononi mwake; Nehemia 6:5 |
Then sent Sanballat his servant to me in like manner the fifth time with an open letter in his hand, |
nayo yakaandikwa humo, Habari imeenea katika mataifa, naye Geshemu asema neno lilo hilo, ya kwamba wewe na Wayahudi mwakusudi kuasi; ndiyo sababu waujenga huo ukuta; nawe wataka kuwamiliki, ndivyo wasemavyo. Nehemia 6:6 |
in which was written, It is reported among the nations, and Gashmu says it, that you and the Jews think to rebel; for which cause you are building the wall: and you would be their king, according to these words. |
Nawe umewaweka manabii ili wakuhubirie huko Yerusalemu, kusema, Yuko mfalme katika Yuda; basi sasa ataarifiwa mfalme sawasawa na maneno haya. Njoo sasa basi, na tufanye shauri pamoja. Nehemia 6:7 |
You have also appointed prophets to preach of you at Jerusalem, saying, There is a king in Judah: and now shall it be reported to the king according to these words. Come now therefore, and let us take counsel together. |
Ndipo mimi nikatuma kwake wajumbe, kusema, Hakukufanyika mambo kama hayo uyasemayo, lakini kwa moyo wako wewe mwenyewe umeyabuni. Nehemia 6:8 |
Then I sent to him, saying, There are no such things done as you say, but you feign them out of your own heart. |
Kwani hao wote walitaka kutuogofisha, wakisema, Italegea mikono yao katika kazi, isifanyike. Lakini sasa nitaitia mikono yangu nguvu. Nehemia 6:9 |
For they all would have made us afraid, saying, Their hands shall be weakened from the work, that it not be done. But now, [God], strengthen you my hands. |
Nikaingia nyumbani kwa Shemaya, mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, aliyekuwa amefungwa; naye akasema, Tukutane nyumbani mwa Mungu, ndani ya hekalu, tukaifunge milango ya hekalu; kwa maana watakuja kukuua; naam, wakati wa usiku watakuja kukuua. Nehemia 6:10 |
I went to the house of Shemaiah the son of Delaiah the son of Mehetabel, who was shut up; and he said, Let us meet together in the house of God, within the temple, and let us shut the doors of the temple: for they will come to kill you; yes, in the night will they come to kill you. |
Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia. Nehemia 6:11 |
I said, Should such a man as I flee? and who is there that, being such as I, would go into the temple to save his life? I will not go in. |
Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri. Nehemia 6:12 |
I discerned, and, behold, God had not sent him; but he pronounced this prophecy against me: and Tobiah and Sanballat had hired him. |
Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie. Nehemia 6:13 |
For this cause was he hired, that I should be afraid, and do so, and sin, and that they might have matter for an evil report, that they might reproach me. |
Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati sawasawa na hayo matendo yao, na yule nabii mke Noadia, na hao manabii waliosalia, waliotaka kuniogofya. Nehemia 6:14 |
Remember, my God, Tobiah and Sanballat according to these their works, and also the prophetess Noadiah, and the rest of the prophets, that would have put me in fear. |
Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na mbili. Nehemia 6:15 |
So the wall was finished in the twenty-fifth [day] of [the month] Elul, in fifty-two days. |
Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu. Nehemia 6:16 |
It happened, when all our enemies heard [of it], that all the nations that were about us feared, and were much cast down in their own eyes; for they perceived that this work was worked of our God. |
Tena siku zile wakuu wa Yuda walimletea Tobia nyaraka nyingi, nazo nyaraka za Tobia zikawafikilia. Nehemia 6:17 |
Moreover in those days the nobles of Judah sent many letters to Tobiah, and [the letters] of Tobiah came to them. |
Kwa maana walikuwa watu wengi katika Yuda waliomwapia, kwa sababu alikuwa mkwewe Shekania, mwana wa Ara; naye Yehohanani mwanawe amemwoa binti Meshulamu, mwana wa Berekia. Nehemia 6:18 |
For there were many in Judah sworn to him, because he was the son-in-law of Shecaniah the son of Arah; and his son Jehohanan had taken the daughter of Meshullam the son of Berechiah as wife. |
Tena waliyanena mema yake mbele yangu, nayo maneno yangu humwambia yeye. Tobia naye akaniletea mimi nyaraka za kuniogofisha. Nehemia 6:19 |
Also they spoke of his good deeds before me, and reported my words to him. Tobiah sent letters to put me in fear. |