Hesabu 26 Swahili & English

Listen/Download Audio
Hesabu 26 (Swahili) Numbers 26 (English)

Ikawa baada ya hilo pigo, Bwana akanena na Musa na Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, na kuwaambia, Hesabu 26:1

It happened after the plague, that Yahweh spoke to Moses and to Eleazar the son of Aaron the priest, saying,

Fanya jumla ya mkutano wote wa wana wa Israeli, tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi, kwa nyumba za baba zao, hao wote katika Israeli wawezao kutoka kuenenda vitani. Hesabu 26:2

Take the sum of all the congregation of the children of Israel, from twenty years old and upward, by their fathers' houses, all who are able to go forth to war in Israel.

Kisha Musa na Eleazari kuhani wakanena nao katika nchi tambarare za Moabu karibu na mto wa Yordani, huko Yeriko, wakawaambia, Hesabu 26:3

Moses and Eleazar the priest spoke with them in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying,

Fanyeni jumla ya watu, tangu umri wa miaka ishirini, na zaidi; kama Bwana alivyomwagiza Musa na wana wa Israeli, hao waliotoka nchi ya Misri. Hesabu 26:4

[Take the sum of the people], from twenty years old and upward; as Yahweh commanded Moses and the children of Israel, that came forth out of the land of Egypt.

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Israeli, wana wa Reubeni; wa Hanoki, jamaa ya Wahanoki; na wa Palu, jamaa ya Wapalu; Hesabu 26:5

Reuben, the firstborn of Israel; the sons of Reuben: [of] Hanoch, the family of the Hanochites; of Pallu, the family of the Palluites;

na wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; na wa Karmi, jamaa ya Wakarmi. Hesabu 26:6

of Hezron, the family of the Hezronites; of Carmi, the family of the Carmites.

Hizi ndizo jamaa za Wareubeni; na hao waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tatu elfu na mia saba na thelathini. Hesabu 26:7

These are the families of the Reubenites; and those who were numbered of them were forty-three thousand seven hundred thirty.

Na wana wa Palu; Eliabu. Hesabu 26:8

The sons of Pallu: Eliab.

Na wana wa Eliabu; Nemueli, na Dathani, na Abiramu. Hawa ndio Dathani na Abiramu waliochaguliwa na mkutano, ambao walishindana na Musa na Haruni katika mkutano wa Kora, hapo waliposhindana na Bwana; Hesabu 26:9

The sons of Eliab: Nemuel, and Dathan, and Abiram. These are that Dathan and Abiram, who were called of the congregation, who strove against Moses and against Aaron in the company of Korah, when they strove against Yahweh,

nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora, mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini, nao wakawa ishara. Hesabu 26:10

and the earth opened its mouth, and swallowed them up together with Korah, when that company died; what time the fire devoured two hundred fifty men, and they became a sign.

Pamoja na hayo, hao wana wa Kora hawakufa. Hesabu 26:11

Notwithstanding, the sons of Korah didn't die.

Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya Wayakini; Hesabu 26:12

The sons of Simeon after their families: of Nemuel, the family of the Nemuelites; of Jamin, the family of the Jaminites; of Jachin, the family of the Jachinites;

wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli, jamaa ya Washauli. Hesabu 26:13

of Zerah, the family of the Zerahites; of Shaul, the family of the Shaulites.

Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili. Hesabu 26:14

These are the families of the Simeonites, twenty-two thousand two hundred.

Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni; Hesabu 26:15

The sons of Gad after their families: of Zephon, the family of the Zephonites; of Haggi, the family of the Haggites; of Shuni, the family of the Shunites;

wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri; Hesabu 26:16

of Ozni, the family of the Oznites; of Eri, the family of the Erites;

wa Arodi, jamaa ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli. Hesabu 26:17

of Arod, the family of the Arodites; of Areli, the family of the Arelites.

Hizi ndizo jamaa za wana wa Gadi kama waliohesabiwa kwao, arobaini elfu na mia tano. Hesabu 26:18

These are the families of the sons of Gad according to those who were numbered of them, forty thousand and five hundred.

Na wana wa Yuda, Eri na Onani; na hao Eri na Onani wakafa katika nchi ya Kanaani. Hesabu 26:19

The sons of Judah: Er and Onan; and Er and Onan died in the land of Canaan.

Na wana wa Yuda kwa jamaa zao; wa Shela, jamaa ya Washela; wa Peresi, jamaa ya Waperesi; wa Zera, jamaa ya Wazera. Hesabu 26:20

The sons of Judah after their families were: of Shelah, the family of the Shelanites; of Perez, the family of the Perezites; of Zerah, the family of the Zerahites.

Na wana wa Peresi walikuwa; wa Hesroni, jamaa ya Wahesroni; wa Hamuli, jamaa ya Wahamuli. Hesabu 26:21

The sons of Perez were: of Hezron, the family of the Hezronites; of Hamul, the family of the Hamulites.

Hizi ndizo jamaa za Yuda kama waliohesabiwa kwao, sabini na sita elfu na mia tano. Hesabu 26:22

These are the families of Judah according to those who were numbered of them, seventy-six thousand five hundred.

Na wana wa Isakari kwa jamaa zao; wa Tola, jamaa ya Watola; wa Puva, jamaa ya Wapuva; Hesabu 26:23

The sons of Issachar after their families: [of] Tola, the family of the Tolaites; of Puvah, the family of the Punites;

wa Yashubu, jamaa ya Wayashubu; wa Shimroni, jamaa ya Washimroni. Hesabu 26:24

of Jashub, the family of the Jashubites; of Shimron, the family of the Shimronites.

Hizi ndizo jamaa za Isakari kama waliohesabiwa kwao, sitini na nne elfu na mia tatu. Hesabu 26:25

These are the families of Issachar according to those who were numbered of them, sixty-four thousand three hundred.

Na wana wa Zabuloni kwa jamaa zao; wa Seredi, jamaa ya Waseredi; wa Eloni, jamaa ya Waeloni; wa Yaleeli, jamaa ya Wayaleeli. Hesabu 26:26

The sons of Zebulun after their families: of Sered, the family of the Seredites; of Elon, the family of the Elonites; of Jahleel, the family of the Jahleelites.

Hizi ndizo jamaa za Wazabuloni kama waliohesabiwa kwao, sitini elfu na mia tano. Hesabu 26:27

These are the families of the Zebulunites according to those who were numbered of them, sixty thousand five hundred.

Na wana wa Yusufu kwa jamaa zao; Manase na Efraimu. Hesabu 26:28

The sons of Joseph after their families: Manasseh and Ephraim.

Wana wa Manase; wa Makiri, jamaa ya Wamakiri; na Makiri akamzaa Gileadi; wa Gileadi, jamaa ya Wagileadi. Hesabu 26:29

The sons of Manasseh: of Machir, the family of the Machirites; and Machir became the father of Gilead; of Gilead, the family of the Gileadites.

Hawa ndio wana wa Gileadi; wa Abiezeri, jamaa ya Waabiezeri; wa Heleki, jamaa ya Waheleki; Hesabu 26:30

These are the sons of Gilead: [of] Iezer, the family of the Iezerites; of Helek, the family of the Helekites;

na wa Asrieli, jamaa ya Waasrieli; na wa Shekemu, jamaa ya Washekemu; Hesabu 26:31

and [of] Asriel, the family of the Asrielites; and [of] Shechem, the family of the Shechemites;

na wa Shemida, jamaa ya Washemida; na wa Heferi, jamaa ya Waheferi. Hesabu 26:32

and [of] Shemida, the family of the Shemidaites; and [of] Hepher, the family of the Hepherites.

Na Selofehadi mwana wa Heferi hakuwa na wana waume, isipokuwa wa kike; na majina ya hao binti za Selofehadi ni haya, Mala, na Noa, na Hogla, na Milka, na Tirsa. Hesabu 26:33

Zelophehad the son of Hepher had no sons, but daughters: and the names of the daughters of Zelophehad were Mahlah, and Noah, Hoglah, Milcah, and Tirzah.

Hizi ndizo jamaa za Manase; na waliohesabiwa kwao walikuwa ni hamsini na mbili elfu na mia saba. Hesabu 26:34

These are the families of Manasseh; and those who were numbered of them were fifty-two thousand seven hundred.

Na wana wa Efraimu kwa jamaa zao; wa Shuthela, jamaa ya Washuthela; wa Beredi, jamaa ya Waberedi; wa Tahathi, jamaa ya Watahathi. Hesabu 26:35

These are the sons of Ephraim after their families: of Shuthelah, the family of the Shuthelahites; of Becher, the family of the Becherites; of Tahan, the family of the Tahanites.

Na wana wa Shuthela ni hawa; wa Erani, jamaa ya Waerani. Hesabu 26:36

These are the sons of Shuthelah: of Eran, the family of the Eranites.

Hizi ndizo jamaa za wana wa Efraimu kama waliohesabiwa kwao, thelathini na mbili elfu na mia tano. Hao ndio wana wa Yusufu kwa jamaa zao. Hesabu 26:37

These are the families of the sons of Ephraim according to those who were numbered of them, thirty-two thousand five hundred. These are the sons of Joseph after their families.

Na wana wa Benyamini kwa jamaa zao; wa Bela, jamaa ya Wabela; na wa Ashbeli, jamaa ya Waashbeli; wa Ahiramu, jamaa ya Waahiramu; Hesabu 26:38

The sons of Benjamin after their families: of Bela, the family of the Belaites; of Ashbel, the family of the Ashbelites; of Ahiram, the family of the Ahiramites;

wa Shufamu, jamaa ya Washufamu; wa Hufamu, jamaa ya Wahufamu. Hesabu 26:39

of Shephupham, the family of the Shuphamites; of Hupham, the family of the Huphamites.

Na wana wa Bela walikuwa Ardi na Naamani; wa Ardi, jamaa ya Waardi; wa Naamani, jamaa ya Wanaamani. Hesabu 26:40

The sons of Bela were Ard and Naaman: [of Ard], the family of the Ardites; of Naaman, the family of the Naamites.

Hao ndio wana wa Benyamini kwa jamaa zao; na waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tano elfu na mia sita. Hesabu 26:41

These are the sons of Benjamin after their families; and those who were numbered of them were forty-five thousand six hundred.

Na wana wa Dani ni hawa kwa jamaa zao; wa Shuhamu, jamaa ya Washuhamu. Hizi ndizo jamaa za Dani kwa jamaa zao. Hesabu 26:42

These are the sons of Dan after their families: of Shuham, the family of the Shuhamites. These are the families of Dan after their families.

Jamaa zote za Washuhamu, kama waliohesabiwa kwao, walikuwa sitini na nne elfu na mia nne. Hesabu 26:43

All the families of the Shuhamites, according to those who were numbered of them, were sixty-four thousand four hundred.

Na wana wa Asheri kwa jamaa zao; wa Imna, jamaa ya Waimna; wa Ishvi jamaa ya Waishvi; wa Beria, jamaa ya Waberia. Hesabu 26:44

The sons of Asher after their families: of Imnah, the family of the Imnites; of Ishvi, the family of the Ishvites; of Beriah, the family of the Berites.

Wa wana wa Beria; wa Heberi, jamaa ya Waheberi; wa Malkieli, jamaa ya Wamalkieli. Hesabu 26:45

Of the sons of Beriah: of Heber, the family of the Heberites; of Malchiel, the family of the Malchielites.

Na jina la binti wa Asheri aliitwa Sera. Hesabu 26:46

The name of the daughter of Asher was Serah.

Hizi ndizo jamaa za wana wa Asheri kama waliohesabiwa kwao, hamsini na tatu elfu na mia nne. Hesabu 26:47

These are the families of the sons of Asher according to those who were numbered of them, fifty-three thousand and four hundred.

Na wana wa Naftali kwa jamaa zake; wa Yaseeli, jamaa ya Wayaseeli; na wa Guni, jamaa ya Waguni; Hesabu 26:48

The sons of Naphtali after their families: of Jahzeel, the family of the Jahzeelites; of Guni, the family of the Gunites;

wa Yeseri, jamaa ya Wayeseri, wa Shilemu jamaa ya Washilemu. Hesabu 26:49

of Jezer, the family of the Jezerites; of Shillem, the family of the Shillemites.

Hizi ndizo jamaa za Naftali kwa jamaa zao; na waliohesabiwa kwao walikuwa arobaini na tano elfu na mia nne. Hesabu 26:50

These are the families of Naphtali according to their families; and those who were numbered of them were forty-five thousand four hundred.

Hao ndio waliohesabiwa katika wana wa Israeli, mia sita na moja elfu, na mia saba na thelathini (601,730). Hesabu 26:51

These are those who were numbered of the children of Israel, six hundred one thousand seven hundred thirty.

Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Hesabu 26:52

Yahweh spoke to Moses, saying,

Watu hawa watagawanyiwa nchi hiyo iwe urithi wao, vile vile kama hesabu ya majina yao ilivyo. Hesabu 26:53

To these the land shall be divided for an inheritance according to the number of names.

Hao waliozidi hesabu yao utawapa urithi zaidi, na hao waliopunguka hesabu yao, utawapa urithi kama upungufu wao; kila mtu kama watu wake walivyohesabiwa, ndivyo atakavyopewa urithi wake. Hesabu 26:54

To the more you shall give the more inheritance, and to the fewer you shall give the less inheritance: to everyone according to those who were numbered of him shall his inheritance be given.

Lakini nchi itagawanywa kwa kura; kwa majina ya kabila za baba zao, ndivyo watakavyopata urithi. Hesabu 26:55

Notwithstanding, the land shall be divided by lot: according to the names of the tribes of their fathers they shall inherit.

Kama kura itakavyokuwa, ndivyo urithi wao utakavyogawanywa kati yao, hao wengi na hao wachache. Hesabu 26:56

According to the lot shall their inheritance be divided between the more and the fewer.

Na hao waliohesabiwa katika Walawi kwa jamaa zao ni hawa; wa Gershoni, jamaa ya Wagershoni; na wa Kohathi, jamaa ya Wakohathi; na wa Merari, jamaa ya Wamerari. Hesabu 26:57

These are those who were numbered of the Levites after their families: of Gershon, the family of the Gershonites; of Kohath, the family of the Kohathites; of Merari, the family of the Merarites.

Hizi ndizo jamaa za Lawi; jamaa ya Walibni, na jamaa ya Wahebroni, na jamaa ya Wamala, na jamaa ya Wamushi jamaa ya Wakora. Na Kohathi alimzaa Amramu. Hesabu 26:58

These are the families of Levi: the family of the Libnites, the family of the Hebronites, the family of the Mahlites, the family of the Mushites, the family of the Korahites. Kohath became the father of Amram.

Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi, binti wa Lawi, ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amramu Haruni, na Musa, na Miriamu umbu lao. Hesabu 26:59

The name of Amram's wife was Jochebed, the daughter of Levi, who was born to Levi in Egypt: and she bore to Amram Aaron and Moses, and Miriam their sister.

Tena kwake Haruni walizaliwa hawa, Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari. Hesabu 26:60

To Aaron were born Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.

Tena Nadabu na Abihu wakafa, hapo waliposongeza moto wa kigeni mbele za Bwana. Hesabu 26:61

Nadab and Abihu died, when they offered strange fire before Yahweh.

Na hao waliohesabiwa kwao walikuwa ishirini na tatu elfu, kila mwanamume tangu huyo aliyepata umri wa mwezi mmoja, na zaidi; kwa kuwa hawakuhesabiwa katika wana wa Israeli, kwa sababu hawakupewa urithi katika wana wa Israeli. Hesabu 26:62

Those who were numbered of them were twenty-three thousand, every male from a month old and upward: for they were not numbered among the children of Israel, because there was no inheritance given them among the children of Israel.

Hao ndio waliohesabiwa na Musa na Eleazari kuhani; ambao waliwahesabu wana wa Israeli katika nchi tambarare za Moabu, karibu na Yordani, hapo Yeriko. Hesabu 26:63

These are those who were numbered by Moses and Eleazar the priest, who numbered the children of Israel in the plains of Moab by the Jordan at Jericho.

Lakini katika watu hao hapakuwa na mtu hata mmoja wa wale waliohesabiwa na Musa na Haruni kuhani; waliowahesabu wana wa Israeli katika bara ya Sinai. Hesabu 26:64

But among these there was not a man of them who were numbered by Moses and Aaron the priest, who numbered the children of Israel in the wilderness of Sinai.

Kwa kuwa Bwana alisema juu yao, Hapana budi watakufa nyikani. Napo hapakusalia mtu mmoja miongoni mwao, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni. Hesabu 26:65

For Yahweh had said of them, They shall surely die in the wilderness. There was not left a man of them, save Caleb the son of Jephunneh, and Joshua the son of Nun.