2 Wakorintho 6 Swahili & English
Listen/Download Audio2 Wakorintho 6 (Swahili) | 2nd Corinthians 6 (English) |
---|---|
Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure. 2 Wakorintho 6:1 |
Working together, we entreat also that you not receive the grace of God in vain, |
(Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa) 2 Wakorintho 6:2 |
for he says, "At an acceptable time I listened to you, In a day of salvation I helped you." Behold, now is the acceptable time. Behold, now is the day of salvation. |
Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe; 2 Wakorintho 6:3 |
We give no occasion of stumbling in anything, that our service may not be blamed, |
bali katika kila neno tujipatie sifa njema, kama watumishi wa Mungu; katika saburi nyingi, katika dhiki, katika misiba, katika shida; 2 Wakorintho 6:4 |
but in everything commending ourselves, as servants of God, in great endurance, in afflictions, in hardships, in distresses, |
katika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika taabu, katika kukesha, katika kufunga; 2 Wakorintho 6:5 |
in beatings, in imprisonments, in riots, in labors, in watchings, in fastings; |
katika kuwa safi, katika elimu, katika uvumilivu, katika utu wema, katika Roho Mtakatifu, katika upendo usio unafiki; 2 Wakorintho 6:6 |
in pureness, in knowledge, in patience, in kindness, in the Holy Spirit, in sincere love, |
katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto; 2 Wakorintho 6:7 |
in the word of truth, in the power of God; by the armor of righteousness on the right hand and on the left, |
kwa utukufu na aibu; kwa kunenwa vibaya na kunenwa vema; kama wadanganyao, bali tu watu wa kweli; 2 Wakorintho 6:8 |
by glory and dishonor, by evil report and good report; as deceivers, and yet true; |
kama wasiojulikana, bali wajulikanao sana; kama wanaokufa, kumbe tu hai; kama wanaorudiwa, bali wasiouawa; 2 Wakorintho 6:9 |
as unknown, and yet well known; as dying, and behold, we live; as punished, and not killed; |
kama wenye huzuni, bali siku zote tu wenye furaha; kama maskini, bali tukitajirisha wengi; kama wasio na kitu, bali tu wenye vitu vyote. 2 Wakorintho 6:10 |
as sorrowful, yet always rejoicing; as poor, yet making many rich; as having nothing, and yet possessing all things. |
Vinywa vyetu vimefumbuliwa kwenu, enyi Wakorintho; mioyo yetu imekunjuliwa. 2 Wakorintho 6:11 |
Our mouth is open to you, Corinthians. Our heart is enlarged. |
Hamsongwi ndani yetu, bali mwasongwa katika mioyo yenu. 2 Wakorintho 6:12 |
You are not restricted by us, but you are restricted by your own affections. |
Basi, ili mlipe kadiri ile mliyopewa (nasema nanyi kama na watoto), nanyi pia mkunjuliwe mioyo. 2 Wakorintho 6:13 |
Now in return, I speak as to my children, you also be open wide. |
Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 2 Wakorintho 6:14 |
Don't be unequally yoked with unbelievers, for what fellowship have righteousness and iniquity? Or what communion has light with darkness? |
Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 2 Wakorintho 6:15 |
What agreement has Christ with Belial? Or what portion has a believer with an unbeliever? |
Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 2 Wakorintho 6:16 |
What agreement has a temple of God with idols? For you are a temple of the living God. Even as God said, "I will dwell in them, and walk in them; and I will be their God, and they will be my people." |
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 2 Wakorintho 6:17 |
Therefore, "'Come out from among them, And be separate,' says the Lord, 'Touch no unclean thing. I will receive you. |
Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike, 2 Wakorintho 6:18 |
I will be to you a Father. You will be to me sons and daughters,' says the Lord Almighty." |