Ayabu 19 Swahili & English
Listen/Download AudioAyabu 19 (Swahili) | Job 19 (English) |
---|---|
Ndipo Ayubu akajibu, na kusema, Ayabu 19:1 |
Then Job answered, |
Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno? Ayabu 19:2 |
"How long will you torment me, And crush me with words? |
Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu. Ayabu 19:3 |
You have reproached me ten times. You aren't ashamed that you attack me. |
Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe. Ayabu 19:4 |
If it is true that I have erred, My error remains with myself. |
Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu; Ayabu 19:5 |
If indeed you will magnify yourselves against me, And plead against me my reproach; |
Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake. Ayabu 19:6 |
Know now that God has subverted me, And has surrounded me with his net. |
Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu. Ayabu 19:7 |
"Behold, I cry out of wrong, but I am not heard: I cry for help, but there is no justice. |
Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu. Ayabu 19:8 |
He has walled up my way so that I can't pass, And has set darkness in my paths. |
Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu. Ayabu 19:9 |
He has stripped me of my glory, And taken the crown from my head. |
Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling'oa kama mti. Ayabu 19:10 |
He has broken me down on every side, and I am gone. My hope he has plucked up like a tree. |
Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake. Ayabu 19:11 |
He has also kindled his wrath against me. He counts me among his adversaries. |
Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu. Ayabu 19:12 |
His troops come on together, Build a siege ramp against me, And encamp around my tent. |
Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa. Ayabu 19:13 |
"He has put my brothers far from me. My acquaintances are wholly estranged from me. |
Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau. Ayabu 19:14 |
My relatives have gone away. My familiar friends have forgotten me. |
Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao. Ayabu 19:15 |
Those who dwell in my house, and my maids, count me for a stranger. I am an alien in their sight. |
Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu. Ayabu 19:16 |
I call to my servant, and he gives me no answer; I beg him with my mouth. |
Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu. Ayabu 19:17 |
My breath is offensive to my wife. I am loathsome to the children of my own mother. |
Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena. Ayabu 19:18 |
Even young children despise me. If I arise, they speak against me. |
Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia. Ayabu 19:19 |
All my familiar friends abhor me. They whom I loved have turned against me. |
Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu. Ayabu 19:20 |
My bones stick to my skin and to my flesh. I have escaped by the skin of my teeth. |
Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa. Ayabu 19:21 |
"Have pity on me, have pity on me, you my friends; For the hand of God has touched me. |
Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu? Ayabu 19:22 |
Why do you persecute me as God, And are not satisfied with my flesh? |
Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni! Ayabu 19:23 |
"Oh that my words were now written! Oh that they were inscribed in a book! |
Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi. Ayabu 19:24 |
That with an iron pen and lead They were engraved in the rock forever! |
Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Ayabu 19:25 |
But as for me, I know that my Redeemer lives. In the end, he will stand upon the earth. |
Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu; Ayabu 19:26 |
After my skin is destroyed, Then in my flesh shall I see God, |
Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu. Ayabu 19:27 |
Whom I, even I, shall see on my side. My eyes shall see, and not as a stranger. "My heart is consumed within me. |
Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake; Ayabu 19:28 |
If you say, 'How we will persecute him!' Because the root of the matter is found in me, |
Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko. Ayabu 19:29 |
Be afraid of the sword, For wrath brings the punishments of the sword, That you may know there is a judgment." |