Ayabu 36 Swahili & English

Listen/Download Audio
Ayabu 36 (Swahili) Job 36 (English)

Tena Elihu akaendelea na kusema, Ayabu 36:1

Elihu also continued, and said,

Ningojee kidogo nami nitakueleza; Kwa kuwa nikali na maneno kwa ajili ya Mungu. Ayabu 36:2

"Bear with me a little, and I will show you; For I still have something to say on God's behalf.

Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali, Nami nitampa haki Muumba wangu. Ayabu 36:3

I will get my knowledge from afar, And will ascribe righteousness to my Maker.

Kwani yakini maneno yangu si ya uongo; Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe. Ayabu 36:4

For truly my words are not false. One who is perfect in knowledge is with you.

Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote; Ana uweza katika nguvu za fahamu. Ayabu 36:5

"Behold, God is mighty, and doesn't despise anyone. He is mighty in strength of understanding.

Hauhifadhi uhai wa waovu; Lakini huwapa wateswao haki yao. Ayabu 36:6

He doesn't preserve the life of the wicked, But gives to the afflicted their right.

Yeye hawaondolei macho yake wenye haki; Lakini pamoja na wafalme huwaweka Katika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa. Ayabu 36:7

He doesn't withdraw his eyes from the righteous, But with kings on the throne, He sets them forever, and they are exalted.

Nao wakifungwa kwa pingu, Wakitwaliwa kwa kamba za mateso; Ayabu 36:8

If they are bound in fetters, And are taken in the cords of afflictions,

Ndipo huwaonyesha matendo yao, Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna. Ayabu 36:9

Then he shows them their work, And their transgressions, that they have behaved themselves proudly.

Yeye huyafunua masikio yao, wasikie maonyo, Na kuwaagiza warudi kuuacha uovu. Ayabu 36:10

He also opens their ears to instruction, And commands that they return from iniquity.

Kama wakisikia na kumtumikia, Watapisha siku zao katika kufanikiwa, Na miaka yao katika furaha. Ayabu 36:11

If they listen and serve him, They shall spend their days in prosperity, And their years in pleasures.

Lakini wasiposikia, wataangamia kwa upanga, Nao watakufa pasipo maarifa. Ayabu 36:12

But if they don't listen, they shall perish by the sword; They shall die without knowledge.

Lakini hao wasiomcha Mungu mioyoni hujiwekea hasira Hawalilii msaada hapo awafungapo. Ayabu 36:13

"But those who are godless in heart lay up anger. They don't cry for help when he binds them.

Wao hufa wakali vijana, Na uhai wao huangamia katikati ya wachafu. Ayabu 36:14

They die in youth. Their life perishes among the unclean.

Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake, Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu. Ayabu 36:15

He delivers the afflicted by their affliction, And opens their ear in oppression.

Naam, yeye angekuongoza utoke katika msiba Hata mahali penye nafasi, ambapo hapana msonge; Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta. Ayabu 36:16

Yes, he would have allured you out of distress, Into a broad place, where there is no restriction. That which is set on your table would be full of fatness.

Lakini umejaa hukumu ya waovu; Hukumu na haki hukushika. Ayabu 36:17

"But you are full of the judgment of the wicked. Judgment and justice take hold of you.

Basi ujitunze, isije hasira ikakuvuta hata ukafanya mzaha; Wala usikubali ukuu wa ukombozi ukugeuze. Ayabu 36:18

Don't let riches entice you to wrath, Neither let the great size of a bribe turn you aside.

Je! Mali yako yatatosha, hata usiwe katika taabu, Au uwezo wote wa nguvu zako? Ayabu 36:19

Would your wealth sustain you in distress, Or all the might of your strength?

Usiutamani usiku, Wakati watu wakatwapo katika mahali pao. Ayabu 36:20

Don't desire the night, When people are cut off in their place.

Jitunze, usiutazame uovu; Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu. Ayabu 36:21

Take heed, don't regard iniquity; For this you have chosen rather than affliction.

Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake; Ni nani afundishaye kama yeye? Ayabu 36:22

Behold, God is exalted in his power. Who is a teacher like him?

Ni nani aliyemwagiza njia yake? Au ni nani awezaye kusema, Wewe umetenda yasiyo haki? Ayabu 36:23

Who has prescribed his way for him? Or who can say, 'You have committed unrighteousness?'

Kumbuka kuitukuza kazi yake, Watu waliyoiimbia. Ayabu 36:24

"Remember that you magnify his work, Whereof men have sung.

Wanadamu wote wameitazama; Watu huiangalia kwa mbali Ayabu 36:25

All men have looked thereon. Man sees it afar off.

Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui; Hesabu ya miaka yake haitafutiki. Ayabu 36:26

Behold, God is great, and we don't know him. The number of his years is unsearchable.

Kwani yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake; Ayabu 36:27

For he draws up the drops of water, Which distill in rain from his vapor,

Ambayo mawingu yainyesha Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi. Ayabu 36:28

Which the skies pour down And drop on man abundantly.

Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu, Ngurumo za makao yake? Ayabu 36:29

Yes, can any understand the spreading of the clouds, And the thunderings of his pavilion?

Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke; Naye hufunika vilindi vya bahari. Ayabu 36:30

Behold, he spreads his light around him. He covers the bottom of the sea.

Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi; Hutoa chakula kwa ukarimu. Ayabu 36:31

For by these he judges the people. He gives food in abundance.

Yeye huifunika mikono yake kwa umeme; Na kuuagiza shabaha utakayopiga. Ayabu 36:32

He covers his hands with the lightning, And commands it to strike the mark.

Mshindo wake hutoa habari zake, Anayewaka hasira juu ya uovu. Ayabu 36:33

The noise of it tells about him, And the cattle also concerning the storm that comes up.