Zaburi 19 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 19 (Swahili) | Psalms 19 (English) |
---|---|
Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono yake. Zaburi 19:1 |
> The heavens declare the glory of God. The expanse shows his handiwork. |
Mchana husemezana na mchana, Usiku hutolea usiku maarifa. Zaburi 19:2 |
Day after day they pour forth speech, And night after night they display knowledge. |
Hakuna lugha wala maneno, Sauti yao haisikilikani. Zaburi 19:3 |
There is no speech nor language, Where their voice is not heard. |
Sauti yao imeenea duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. Katika hizo ameliwekea jua hema, Zaburi 19:4 |
Their voice has gone out through all the earth, Their words to the end of the world. In them he has set a tent for the sun, |
Kama bwana arusi akitoka chumbani mwake, Lafurahi kama mtu aliye hodari Kwenda mbio katika njia yake. Zaburi 19:5 |
Which is as a bridegroom coming out of his chamber, Like a strong man rejoicing to run his course. |
Kutoka kwake lautoka mwisho wa mbingu, Na kuzunguka kwake hata miisho yake, Wala kwa hari yake Hakuna kitu kilichositirika. Zaburi 19:6 |
His going forth is from the end of the heavens, His circuit to its ends; There is nothing hidden from its heat. |
Sheria ya Bwana ni kamilifu, Huiburudisha nafsi. Ushuhuda wa Bwana ni amini, Humtia mjinga hekima. Zaburi 19:7 |
Yahweh's law is perfect, restoring the soul. Yahweh's testimony is sure, making wise the simple. |
Maagizo ya Bwana ni ya adili, Huufurahisha moyo. Amri ya Bwana ni safi, Huyatia macho nuru. Zaburi 19:8 |
Yahweh's precepts are right, rejoicing the heart. Yahweh's commandment is pure, enlightening the eyes. |
Kicho cha Bwana ni kitakatifu, Kinadumu milele. Hukumu za Bwana ni kweli, Zina haki kabisa. Zaburi 19:9 |
The fear of Yahweh is clean, enduring forever. Yahweh's ordinances are true, and righteous altogether. |
Ni za kutamanika kuliko dhahabu, Kuliko wingi wa dhahabu safi. Nazo ni tamu kuliko asali, Kuliko sega la asali. Zaburi 19:10 |
More to be desired are they than gold, yes, than much fine gold; Sweeter also than honey and the extract of the honeycomb. |
Tena mtumishi wako huonywa kwazo, Katika kuzishika kuna thawabu nyingi. Zaburi 19:11 |
Moreover by them is your servant warned. In keeping them there is great reward. |
Ni nani awezaye kuyatambua makosa yake? Unitakase na mambo ya siri. Zaburi 19:12 |
Who can discern his errors? Forgive me from hidden errors. |
Umzuie mtumishi wako asitende mambo ya kiburi, Yasinitawale mimi. Ndipo nitakapokuwa kamili, Nami nitakuwa safi, sina kosa lililo kubwa. Zaburi 19:13 |
Keep back your servant also from presumptuous sins. Let them not have dominion over me. Then I will be upright, I will be blameless and innocent of great transgression. |
Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu. Zaburi 19:14 |
Let the words of my mouth and the meditation of my heart Be acceptable in your sight, Yahweh, my rock, and my redeemer. |