Zaburi 73 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 73 (Swahili) | Psalms 73 (English) |
---|---|
Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, Kwa hao walio safi mioyo yao. Zaburi 73:1 |
> Surely God is good to Israel, To those who are pure in heart. |
Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza. Zaburi 73:2 |
But as for me, my feet were almost gone. My steps had nearly slipped. |
Maana naliwaonea wivu wenye kujivuna, Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki. Zaburi 73:3 |
For I was envious of the arrogant, When I saw the prosperity of the wicked. |
Maana hawana maumivu katika kufa kwao, Na mwili wao una nguvu. Zaburi 73:4 |
For there are no struggles in their death, But their strength is firm. |
Katika taabu ya watu hawamo, Wala hawapati mapigo pamoja na wanadamu. Zaburi 73:5 |
They are free from burdens of men, Neither are they plagued like other men. |
Hivyo kiburi kimekuwa mkufu shingoni mwao, Jeuri huwavika kama nguo. Zaburi 73:6 |
Therefore pride is like a chain around their neck. Violence covers them like a garment. |
Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao. Zaburi 73:7 |
Their eyes bulge with fat. Their minds pass the limits of conceit. |
Hudhihaki, husimulia mabaya, Husimulia udhalimu kana kwamba wako juu. Zaburi 73:8 |
They scoff and speak with malice. In arrogance, they threaten oppression. |
Wameweka kinywa chao mbinguni, Na ulimi wao hutanga-tanga duniani. Zaburi 73:9 |
They have set their mouth in the heavens. Their tongue walks through the earth. |
Kwa hiyo watu wake hugeuka huko, Na maji yaliyojaa humezwa nao. Zaburi 73:10 |
Therefore their people return to them, And they drink up waters of abundance. |
Nao husema, Mungu ajuaje? Yako maarifa kwake aliye juu? Zaburi 73:11 |
They say, "How does God know? Is there knowledge in the Most High?" |
Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi. Zaburi 73:12 |
Behold, these are the wicked. Being always at ease, they increase in riches. |
Hakika nimejisafisha moyo wangu bure, Nimenawa mikono yangu kwa kutokukosa. Zaburi 73:13 |
Surely in vain I have cleansed my heart, And washed my hands in innocence, |
Maana mchana kutwa nimepigwa, Na kuadhibiwa kila asubuhi. Zaburi 73:14 |
For all day long have I been plagued, And punished every morning. |
Kama ningalisema, Nitasimulia kama hayo; Kumbe! Ningaliwadanganya kizazi cha wana wako. Zaburi 73:15 |
If I had said, "I will speak thus;" Behold, I would have betrayed the generation of your children. |
Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; Ikawa taabu machoni pangu; Zaburi 73:16 |
When I tried to understand this, It was too painful for me; |
Hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu, Nikautafakari mwisho wao. Zaburi 73:17 |
Until I entered God's sanctuary, And considered their latter end. |
Hakika Wewe huwaweka penye utelezi, Huwaangusha mpaka palipoharibika. Zaburi 73:18 |
Surely you set them in slippery places. You throw them down to destruction. |
Namna gani wamekuwa ukiwa mara! Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho. Zaburi 73:19 |
How they are suddenly destroyed! They are completely swept away with terrors. |
Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka, Uondokapo utaidharau sanamu yao. Zaburi 73:20 |
As a dream when one wakes up, So, Lord, when you awake, you will despise their fantasies. |
Moyo wangu ulipoona uchungu, Viuno vyangu viliponichoma, Zaburi 73:21 |
For my soul was grieved. I was embittered in my heart. |
Nalikuwa kama mjinga, sijui neno; Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako. Zaburi 73:22 |
I was so senseless and ignorant. I was a brute beast before you. |
Walakini mimi ni pamoja nawe daima, Umenishika mkono wa kuume. Zaburi 73:23 |
Nevertheless, I am continually with you. You have held my right hand. |
Utaniongoza kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu. Zaburi 73:24 |
You will guide me with your counsel, And afterward receive me to glory. |
Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe. Zaburi 73:25 |
Who do I have in heaven? There is no one on earth who I desire besides you. |
Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele. Zaburi 73:26 |
My flesh and my heart fails, But God is the strength of my heart and my portion forever. |
Maana wajitengao nawe watapotea; Umewaangamiza wote waliokuacha Wewe. Zaburi 73:27 |
For, behold, those who are far from you shall perish. You have destroyed all those who are unfaithful to you. |
Nami kumkaribia Mungu ni kwema kwangu; Nimefanya kimbilio kwa Bwana MUNGU, Niyahubiri matendo yako yote. Zaburi 73:28 |
But it is good for me to come close to God. I have made the Lord Yahweh my refuge, That I may tell of all your works. |