Zaburi 78 Swahili & English
Listen/Download AudioZaburi 78 (Swahili) | Psalms 78 (English) |
---|---|
Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu. Zaburi 78:1 |
> Hear my law, my people. Turn your ears to the words of my mouth. |
Na nifunue kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale. Zaburi 78:2 |
I will open my mouth in a parable. I will utter dark sayings of old, |
Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, Ambayo baba zetu walituambia. Zaburi 78:3 |
Which we have heard and known, And our fathers have told us. |
Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za Bwana, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya. Zaburi 78:4 |
We will not hide them from their children, Telling to the generation to come the praises of Yahweh, His strength, and his wondrous works that he has done. |
Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao, Zaburi 78:5 |
For he established a testimony in Jacob, And appointed a law in Israel, Which he commanded our fathers, That they should make them known to their children; |
Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao Zaburi 78:6 |
That the generation to come might know, even the children who should be born; Who should arise and tell their children, |
Wamwekee Mungu tumaini lao. Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, Bali wazishike amri zake. Zaburi 78:7 |
That they might set their hope in God, And not forget the works of God, But keep his commandments, |
Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu. Zaburi 78:8 |
And might not be as their fathers, A stubborn and rebellious generation, A generation that didn't make their hearts loyal, Whose spirit was not steadfast with God. |
Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, Walirudi nyuma siku ya vita. Zaburi 78:9 |
The children of Ephraim, being armed and carrying bows, Turned back in the day of battle. |
Hawakulishika agano la Mungu; Wakakataa kuenenda katika sheria yake; Zaburi 78:10 |
They didn't keep God's covenant, And refused to walk in his law. |
Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha. Zaburi 78:11 |
They forgot his doings, His wondrous works that he had shown them. |
Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani. Zaburi 78:12 |
He did marvelous things in the sight of their fathers, In the land of Egypt, in the field of Zoan. |
Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu. Zaburi 78:13 |
He split the sea, and caused them to pass through; He made the waters stand as a heap. |
Akawaongoza kwa wingu mchana, Na usiku kucha kwa nuru ya moto. Zaburi 78:14 |
In the daytime he also led them with a cloud, And all night with a light of fire. |
Akapasua miamba jangwani; Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi. Zaburi 78:15 |
He split rocks in the wilderness, And gave them drink abundantly as out of the depths. |
Akatokeza na vijito gengeni, Akatelemsha maji kama mito. Zaburi 78:16 |
He brought streams also out of the rock, And caused waters to run down like rivers. |
Lakini wakazidi kumtenda dhambi, Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu. Zaburi 78:17 |
Yet they still went on to sin against him, To rebel against the Most High in the desert. |
Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao. Zaburi 78:18 |
They tempted God in their heart By asking food according to their desire. |
Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani? Zaburi 78:19 |
Yes, they spoke against God. They said, "Can God prepare a table in the wilderness? |
Tazama, aliupiga mwamba; Maji yakabubujika, ikafurika mito. Pia aweza kutupa chakula? Atawaandalia watu wake nyama? Zaburi 78:20 |
Behold, he struck the rock, so that waters gushed out, Streams overflowed. Can he give bread also? Will he provide flesh for his people?" |
Hivyo Bwana aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli. Zaburi 78:21 |
Therefore Yahweh heard, and was angry. A fire was kindled against Jacob, Anger also went up against Israel, |
Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, Wala hawakuutumainia wokovu wake. Zaburi 78:22 |
Because they didn't believe in God, And didn't trust in his salvation. |
Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni; Zaburi 78:23 |
Yet he commanded the skies above, And opened the doors of heaven. |
Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni. Zaburi 78:24 |
He rained down manna on them to eat, And gave them food from the sky. |
Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha. Zaburi 78:25 |
Man ate the bread of angels. He sent them food to the full. |
Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; Akaiongoza kusi kwa uweza wake. Zaburi 78:26 |
He caused the east wind to blow in the sky. By his power he guided the south wind. |
Akawanyeshea nyama kama mavumbi, Na ndege wenye mbawa, Kama mchanga wa bahari. Zaburi 78:27 |
He rained also flesh on them as the dust; Winged birds as the sand of the seas. |
Akawaangusha kati ya matuo yao, Pande zote za maskani zao. Zaburi 78:28 |
He let them fall in the midst of their camp, Around their habitations. |
Wakala wakashiba sana; Maana aliwaletea walivyovitamani; Zaburi 78:29 |
So they ate, and were well filled. He gave them their own desire. |
Hawakuachana na matakwa yao. Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao Zaburi 78:30 |
They didn't turn from their cravings. Their food was yet in their mouths, |
Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli. Zaburi 78:31 |
When the anger of God went up against them, Killed some of the fattest of them, And struck down the young men of Israel. |
Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu. Zaburi 78:32 |
For all this they still sinned, And didn't believe in his wondrous works. |
Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha. Zaburi 78:33 |
Therefore he consumed their days in vanity, And their years in terror. |
Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii. Zaburi 78:34 |
When he killed them, then they inquired after him. They returned and sought God earnestly. |
Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao. Zaburi 78:35 |
They remembered that God was their rock, The Most High God their redeemer. |
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao. Zaburi 78:36 |
But they flattered him with their mouth, And lied to him with their tongue. |
Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake. Zaburi 78:37 |
For their heart was not right with him, Neither were they faithful in his covenant. |
Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote. Zaburi 78:38 |
But he, being merciful, forgave iniquity, and didn't destroy them. Yes, many times he turned his anger away, And didn't stir up all his wrath. |
Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi. Zaburi 78:39 |
He remembered that they were but flesh, A wind that passes away, and doesn't come again. |
Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani! Zaburi 78:40 |
How often they rebelled against him in the wilderness, And grieved him in the desert! |
Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli. Zaburi 78:41 |
They turned again and tempted God, And provoked the Holy One of Israel. |
Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi. Zaburi 78:42 |
They didn't remember his hand, Nor the day when he redeemed them from the adversary; |
Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani. Zaburi 78:43 |
How he set his signs in Egypt, His wonders in the field of Zoan, |
Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa. Zaburi 78:44 |
Turned their rivers into blood, And their streams, so that they could not drink. |
Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu. Zaburi 78:45 |
He sent among them swarms of flies, which devoured them; And frogs, which destroyed them. |
Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao. Zaburi 78:46 |
He gave also their increase to the caterpillar, And their labor to the locust. |
Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu. Zaburi 78:47 |
He destroyed their vines with hail, Their sycamore-fig trees with frost. |
Akaacha ng'ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme. Zaburi 78:48 |
He gave over their cattle also to the hail, And their flocks to hot thunderbolts. |
Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya. Zaburi 78:49 |
He threw on them the fierceness of his anger, Wrath, indignation, and trouble, And a band of angels of evil. |
Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao; Zaburi 78:50 |
He made a path for his anger. He didn't spare their soul from death, But gave their life over to the pestilence, |
Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu. Zaburi 78:51 |
And struck all the firstborn in Egypt, The chief of their strength in the tents of Ham. |
Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani. Zaburi 78:52 |
But he led forth his own people like sheep, And guided them in the wilderness like a flock. |
Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao. Zaburi 78:53 |
He led them safely, so that they weren't afraid, But the sea overwhelmed their enemies. |
Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume. Zaburi 78:54 |
He brought them to the border of his sanctuary, To this mountain, which his right hand had taken. |
Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao. Zaburi 78:55 |
He also drove out the nations before them, Allotted them for an inheritance by line, And made the tribes of Israel to dwell in their tents. |
Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake. Zaburi 78:56 |
Yet they tempted and rebelled against the Most High God, And didn't keep his testimonies; |
Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa. Zaburi 78:57 |
But turned back, and dealt treacherously like their fathers. They were turned aside like a deceitful bow. |
Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao. Zaburi 78:58 |
For they provoked him to anger with their high places, And moved him to jealousy with their engraved images. |
Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa. Zaburi 78:59 |
When God heard this, he was angry, And greatly abhorred Israel; |
Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu; Zaburi 78:60 |
So that he forsook the tent of Shiloh, The tent which he placed among men; |
Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi. Zaburi 78:61 |
And delivered his strength into captivity, His glory into the adversary's hand. |
Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; Akaughadhibikia urithi wake. Zaburi 78:62 |
He also gave his people over to the sword, And was angry with his inheritance. |
Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi, Zaburi 78:63 |
Fire devoured their young men; Their virgins had no wedding song. |
Makuhani wao walianguka kwa upanga, Wala wajane wao hawakuomboleza. Zaburi 78:64 |
Their priests fell by the sword, And their widows couldn't weep. |
Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo; Zaburi 78:65 |
Then the Lord awakened as one out of sleep, Like a mighty man who shouts by reason of wine. |
Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, Akawatia aibu ya milele. Zaburi 78:66 |
He struck his adversaries backward. He put them to a perpetual reproach. |
Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila ya Efraimu. Zaburi 78:67 |
Moreover he rejected the tent of Joseph, And didn't choose the tribe of Ephraim, |
Bali aliichagua kabila ya Yuda, Mlima Sayuni alioupenda. Zaburi 78:68 |
But chose the tribe of Judah, Mount Zion which he loved. |
Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele. Zaburi 78:69 |
He built his sanctuary like the heights, Like the earth which he has established forever. |
Akamchagua Daudi, mtumishi wake, Akamwondoa katika mazizi ya kondoo. Zaburi 78:70 |
He also chose David his servant, And took him from the sheepfolds; |
Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake. Zaburi 78:71 |
From following the ewes that have their young, He brought him to be the shepherd of Jacob, his people, And Israel, his inheritance. |
Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake. Zaburi 78:72 |
So he was their shepherd according to the integrity of his heart, And guided them by the skillfulness of his hands. |